Madaktari Kaunti ya Kilifi wawatoza waathiriwa wa ukatili wa kijinsia Sh3,000 kwa fomu za P3
Da ktari katika Kituo cha Afya cha Ganze mnamo siku ya Ijumanne tarehe 29 Machi, alikataa kugonga muhuri fomu ya P3 ya Grace Charo, ambaye ana ujauzito wa miezi mitano, kwa kukosa kulipa Sh3,000. Bi Charo kutoka kijiji cha Tsangalaweni katika Kaunti ndogo ya Ganze, alikuwa ameripoti kesi katika kituo cha polisi kuwa mumewe alikuwa amempiga na kumjeruhi. Kesi hiyo ilirekodiwa chini ya OB/04/29/3/22 katika kituo cha polisi cha Ganze na pia Bi Charo pia aliomba usaidizi kutoka kwa washawishi Sauti ya Wanawake. “Alifika katika kituo cha polisi kuripoti suala hilo, kisha akaja nikamsaidia kwenda hospitali. Uso wake ulikuwa umevimba, akiwa na majeraha na mwili wake ukiwa na damu,” alisema mwenyekiti wa ukumbi huo Judith Uchi. Bi Uchi alisema walikwenda katika Kituo cha Afya cha Ganze kwa matibabu, lakini afisa mmoja katika kituo cha GBV akaomba Sh3,000. “Nilisisitiza kuwa mwathiriwa alikuwa katika mazingira magumu na hawezi kumudu fedha hizo, na baada ya yote, kesi hiyo ilikuwa ni suala la U...